TUMUSIFU BWANA

prop

Friday 8 June 2018

BUNGE LAIZUNGUMZIA SIMBA LEO KWA KUFIKA FAINAL SPORT PESA CUP WASEMA HAYA

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.


Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe, amewapongeza Simba kufanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup nchini Kenya.

Simba imefanikiwa kufika hatua hiyo baada ya ushindi wa changamoto ya mikwaju ya penati wa mabao 5-4 dhidi ya Kakamega HomeBoyz FC ikiwa ni baada ya dakika 90 kumalizka kwa sare tasa ya 0-0.

Akizungumza bungeni mjini Dodoma, Mwakyembe amefunguka na kueleza Simba wamethibitisha kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Vodacom si kwa kubahatisha mpaka kufikia hatua hiyo ya kucheza fainali na Gor Mahia.

"Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Simba kwa kufanikiwa kutinga fainali ya SportPesa Super Kenya, wamethibitisha kuwa walichukua ubingwa wa ligi si kwa kubahatisha kwa soka la kiwango" amesema.

Mchezo wa fainali ya mashindano hayo utachezwa kwenye Uwanja uleule wa Afraha Jumapili ya wiki hii ambapo bingwa wa michuano hiyo atacheza dhidi ya Everton kwenye Uwanja wa Goodison Park nchini England.

No comments:

Post a Comment