Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Mtibwa Sugar imeendeleza sera zake za kulea vipaji vya wanasoka chipukizi, baada ya kumsainisha mkataba mpya wa miaka miwili, beki wa kulia, Kibwana Ally Shomary.
Katibu Msaidizi wa Mtibwa Sugar, Abubakar Swabur kwamba Shomary amesaini mkataba huo mpya kufuatia mkataba wake wa awali wa miaka miwili pia kukaribia kumalizika.
Mchezaji huyo, zao la timu ya vijana ya Mtibwa Sugar msimu huu amecheza mechi mbili za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika kikosi cha kwanza na zote amefanya vizuri.
BILA MASHABIKI, YANGA KUISHTUA FAR RABAT
11 hours ago

No comments:
Post a Comment