TUMUSIFU BWANA

prop

Thursday 31 May 2018

May 31, 2018

Video Mpya ya Diamond Platnumz ft Rayvanny – Iyena

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.

Bofya APA Ku Download

 Soma hapa kisa cha mtu alie fufuka baada ya mke kufunga siku tisa
May 31, 2018

KURASA MBALIMBALI ZA MAGAZETI YA MICHEZO ,UDAKU NA BURUDANI IJUMAA YA KWANZA YA TAREE 1 .JUNE 2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
 
Kurasa MBALIMBALI za magazeti ya michezo na burudani udaku 




















Endelea kufatilia kalambonews tutakukamilishia magazeti yote ivi punde
May 31, 2018

MFAHAMU MTU ARIYE FARIKI ,KUZIKWA NA KURUDI NYUMBANI

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
AFARIKI, AZIKWA, ARUDI NYUMBANI


ARUSHA: Hali ya taharuki imewakumba wakazi wa Kijiji cha Leto-Mamsera, Kata ya Makidi, Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro kufuatia tukio la mkazi mmoja wa eneo hilo aliyekuwa amefariki dunia miezi miwili iliyopita kuibuka ghafla nyumbani kwake ikielezwa kuwa amefufuka.
Hizi APA kurasa za magazeti juni moja 2018
Marehemu huyo aliyetajwa kwa jina la Richard David Tarimo (28) alifariki kifo cha kutatanisha Machi 30, mwaka huu baada kula nyama aliyoletewa na ndugu yake mmoja na baadaye kuanza kujisikia vibaya na kufariki dunia ghafla wakati akikimbizwa hospitalini kwa matibabu.

MSIKIE MKEWE
Mke wa marehemu aitwaye Mary Richard alieleza kuwa siku ya mazishi ya mumewe huyo kuliibuka jambo la kushangaza kutokana na udongo uliochimbwa kwenye kaburi hilo kutotosha baada ya kulifukia.
Kutokana na hali hiyo, padri aliyekuwa akiongoza misa ya kumwombea marehemu wakati wa mazishi hayo, alihoji kwa nini kaburi halijai udongo ndipo baadhi ya waombolezaji walipomjibu kuwa haliwezi kujaa kwa sababu marehemu amechukuliwa kimazingara.

Mke huyo alisema wiki mbili baada ya marehemu kuzikwa amekuwa akimtokea mkewe barabarani mara kwa mara na kumtaka afunge Novena kwa siku tisa kwani huko aliko anateseka.
Mary alisema kuwa Mei 20, mwaka huu marehemu mumewe aliibuka ghafla ‘laivu’ nyumbani kwake, jambo lililomshangaza na watu wengine kupigwa butwaa baada ya kudaiwa kufufuka.

“Niliamua kufunga Novena na baada ya kumaliza mfungo wa siku tisa ndipo ghafla akatokea mchungaji mmoja ambaye sikuwa namfahamu na kunieleza kuwa marehemu mume wako atarejea.
“Siku iliyofuata marehemu mume wangu aliibuka nyumbani kwangu lakini hakuwa anaongea chochote, alikuwa hajitambui ndipo watu wengi wakiwemo majirani walipojitokeza na kuanza kumshangaa huku wengine wakitaka kumgusa kuona kama kweli alikuwa ni binadamu wa kawaida,” alisema Mary.

TAHARUKI KWA WANANCHI
Hata hivyo, hali ya taharuki iliibuka nyumbani hapo baada ya wananchi kutaka atolewe nje wamwangalie, jambo lililowalazimu wachungaji walioitwa eneo hilo kwa ajili ya kumuombea, kuondoka na mume huyo wa mtu aliyefufuka ambapo alienda kuhifadhiwa nyumbani kwa wachungaji kwa ajili ya maombezi.
Mei 22 mwaka huu, ndipo Richard alipofika nyumbani hapo akiwa anaongea na kumuuliza mkewe hali ya watoto wake na kutaka abandikiwe maji ya kuoga.

Hata hivyo, mkewe alimpatia chakula na alipomaliza kula alipelekewa maji na kuoga na baadaye jioni majira ya saa 10 alitoweka nyumbani katika mazingira ya utata bila kuaga.
“Mei 22 mwaka huu, mume wangu alikuja na kuniuliza hali ya mtoto wake nilimjibu hajambo akaomba nimbandikie maji ya kuoga, nilimpatia chakula kwanza kisha akaenda kuoga na alipomaliza kuoga alivaa nguo zake akatoweka. Lakini baadaye nikaambiwa amerudi kule kwa wachungaji,’’ alisema Mary.

Mamia ya wakazi wa kijiji hicho waliokuwa wamefurika nyumbani kwa marehemu walilizingira kaburi la lake wakitaka lifukuliwe ili waangalie walichozika baada ya marehemu kuonekana akiwa hai ndani ya miezi miwili.
Hata hivyo, hadi mwandishi wetu anaondoka eneo la tukio, wananchi hao hawakufukua kaburi hilo kwa kile kilichoelezwa kuwa hadi wapate kibali cha mahakama.

BABA MZAZI ANASEMAJE?
Baba mzazi wa kijana aliyefufuka, mzee David Kimario ameshangazwa na kurejea kwa mwanaye nyumbani baada ya kudaiwa kufufuka kwani alikufa na wakamzika lakini alisema amefurahi kumpata tena kijana wake kwa sababu kifo chake kilikuwa cha utata na kilitokea ghafla.
“Ninachotaka kujua kwa sasa ni kwamba mwanangu alikuwa wapi na alikuwa akifanya nini na kwenye kaburi tulizika nini?” alihoji mzee Kimario.
Habari zilizotufikia wakati tunakwenda mitamboni zinasema Richard sasa hivi karejea nyumbani kwake na yupo vizuri.

MKUU WA WILAYA ANENA
Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Agness Hokororo akizungumzia suala hilo amesema kwamba mara baada ya kulisikia tukio hilo aliamua kutuma kamati yake ya ulinzi na usalama ya wilaya kwenda eneo hilo.
“Kamati ilifika na kukuta umati uliokuwa na shauku ya kumwona marehemu aliyefufuka,” alis
May 31, 2018

BRITISH HEADLINES NEWSPEPARS ON JUNE 1.2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
 Install kalambonews app to get dairy worlds hot news now











FRIDAY 1ST JUNE 2018
Australia
12:00
Czech Rep
South Korea
12:00
Bos-Herze
Georgia
18:00
Malta
Tunisia
19:15
Turkey
France
20:00
Italy
Egypt
20:15
Colombia
View all International Friendlies scores


May 31, 2018

LULU AENDELEA KUMCHANGANYA BAHATI KUTOKA KENYA

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Bado Lulu ‘anamchanganya’ Bahati kutoka Kenya

1
Kitendo cha Elizabeth Michael ‘Lulu’ kumuweka msanii Bahati kutokea Kenya hotelini kinyume na makubaliano yao, bado hakimtoki kichwani muimbaji huo wa gospel.

Kwa mujibu wa Bahari mwaka 2016 alikuja Tanzania kwa ajili ya kufanya video ya wimbo wake ‘Maria’ na alipanga kumtumia Lulu kama video vixen, hata hivyo mrembo huyo hakutokea katika kikao walichopanga kingefanyika hotelini.

Kwa sasa Bahati amerudi tena Tanzania kwa ajili ya kufanya kazi na msanii wa WCB, Mbosso, hata hivyo bado anakumbuka alichofanyiwa na Lulu.

“Ilikuwa meeting ya video vixen, kama alinifanyia hivyo je anayempenda inakuwaje?, na mimi nilikuwa nimeweka shilingi kidogo, naongea kwa uchungu,” amesema Bahati hapo jana mara alipowasili Bongo.

Soma Pia; Bahati asimulia kilichomtokea kwa Lulu

Hata hivyo baada ya kutompata Lulu, Bahati alikuja kufanya video hiyo na Jokate Mwegelo.

Kabla ya tukio hilo kutokea, hapo awali muimbaji huyo aliwahi kueleza hisia zake kwa Lulu kupitia vyombo vya habari kwa kueleza kuwa iwapo atampata mrembo huyo atakuwa ametulia kabisa.

Loading...

Bofya hapa kusoma habari mbalimbaliSOURCE
BONGO5 ;SOURCES
May 31, 2018

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA ALHAMISI YA 31.2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.


Manchester United wanataka kusaini mkataba mchezaji wa safu ya mashambulizi wa kikosi cha West Marko Arnautovic - the Hammers wanataka mlipo ya pauni £50m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 raia wa Australia. (Sky Sports)
Lakini West Ham inasema hawataki kumuuza mshambuliaji huyo msimu huu . (Evening Standard)
Mo Salah kushiriki katika kombe la dunia Urusi
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho alionekana katika mchezo wa kirafiki Jumatano baina ya Austria na Urusi , mchezo ambao aliucheza Arnautovic. (Vivaro News)
Chelsea wanamfuatilia kwa karibu mshambuliaji kutoka Poland Robert Lewandowski mwenye umri wa miaka 29 baada ya kutangaza kuwa anataka kuondoka Bayern Munich. (Mirror)


Meneja wa Manchester United Jose Mourinho alionekana kwenye mechi iliyomuhusisha Arnautovic, huku kukiwa na fununu kwamba anamtaka kikosini
Liverpool inataka kumuuza mshambuliaji wao Mfaransa Nabil Fekir mwenye umri wa miaka 24 kwa Lyon kwa euro milioni 60m (Le Parisien)
Na the Reds wanae mlindalango wa Barcelona Jasper Cillessen raia wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 29 kwenye orodha yake ya wachezaji wake. (Mundo Deportivo)
Bolt ajiandaa kukabili Mo Farah katika soka Old Trafford
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Italia Jorginho, mwenye umri wa miaka 26, yuko tayari kujiunga na kikosi cha Manchester City kutoka Napoli baada ya kununuliwa kwa euro milioni hamsini 50m baaada ya kukubali mkataba wa miaka mitano na Man city .

BBC: Sources

Wednesday 30 May 2018

May 30, 2018

TETESI ZA USAJILI TANZANIA ALHAMISI YA 31 .2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.

Baada ya kuenea kwa tetesi mbaimbali zikidai kuwa club ya Yanga SC sasa wameyumba kiuchumia kiasi cha kushindwa kufanya usajili wa nafasi tatu za wachezaji watakaoongeza nguvu katika kikosi cha Kombe la shirikisho Afrika.
Soma habari za udaku ,michezo naburudani Leo hapa
Jumatano ya May 30 2018 kutoka mtandao wa habari za michezo wa shaffihdauda.com zimeripotiwa taarifa za kufanya usajili wa mshambuliaji wao wa zamani Mrisho Khalfan Ngassa, Yanga imemsajili Mrisho Ngassa kwa ajili ya kuongeza nguvu.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Mrisho Khalfan Ngassa aliwahi kuichezea Yanga kwa miaka kadhaa kabla ya kuamua kwenda Free State ya Afrika Kusini, Fanja FC ya Oman, Mbeya City ya Mbeya na baadae akajiunga na Ndanda FC kabla ya leo hii kutangazwa kurudi Yanga.

Milardiayo: source
May 30, 2018

KURASA ZA MAGAZETI YA UDAKU,MICHEZO NA BURUDANI ALHAMISI YA TAREE 31 2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
 Kurasa za magazeti ya udaku ,michezo na burudani alhamisi ya taree 31.2018
DOWNLOAD WIMBO MPYA WA AMBWENE MWANSONGWE APA