TUMUSIFU BWANA

prop

Wednesday 28 March 2018

Kroos aikosoa timu ya ujerumani zidi ya kipigo cha Brazilian jana

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Kroos ndiye mshindi wa karibuni wa kombe la dunia kuikemea timu ya Ujerumani kwa uchezaji mbovu, baada ya goli la kipindi cha kwanza la Gabriel Jesus kuihakikishia Brazil ushindi wa 1-0 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Jumanne usiku mjini Berlin.

Baada ya Jerome Boateng kucharuka na kusema "kila kitu" kinahitaji kuboreshwa kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Uhispania siku ya Ijumaa, Kroos naye pia ameshindilia.

"Tulikuwa na baadhi ya wachezaji uwanjani ambao walikuwa na fursa ya kujionyesha kwa ngazi hii - lakini hawakutumia fursa hiyo," Kroos alilalamika, na kuongeza kuwa "tuliruhusu kudhibitiwa na kisha tuliona kwamba hatuko vizuri kama tunavyoambiwa kila mara - na pengine baadhi yetu tunavyodhani tupo."

Kipigo hicho cha nyumbani kiliwagharimu mabingwa hao wa dunia rekodi yako ya kutofungwa kwa mechi 22 mfululizo inayoanzia kwenye kipigo cha Ufaransa katika nusu fainali ya michuano ya kombe la Ulaya ya 2016.

Kwa sare zilizotangulia dhidi ya Uingereza, Ufaransa na Uhispania, Wajerumani wameshindwa kupata ushindi katika mechi zao nne zilizopita -- hali inayozusha wasiwasi mnamo wakati kombe la dunia linakaribia.

No comments:

Post a Comment