TUMUSIFU BWANA

prop

Thursday 31 May 2018

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA ALHAMISI YA 31.2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.


Manchester United wanataka kusaini mkataba mchezaji wa safu ya mashambulizi wa kikosi cha West Marko Arnautovic - the Hammers wanataka mlipo ya pauni £50m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 raia wa Australia. (Sky Sports)
Lakini West Ham inasema hawataki kumuuza mshambuliaji huyo msimu huu . (Evening Standard)
Mo Salah kushiriki katika kombe la dunia Urusi
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho alionekana katika mchezo wa kirafiki Jumatano baina ya Austria na Urusi , mchezo ambao aliucheza Arnautovic. (Vivaro News)
Chelsea wanamfuatilia kwa karibu mshambuliaji kutoka Poland Robert Lewandowski mwenye umri wa miaka 29 baada ya kutangaza kuwa anataka kuondoka Bayern Munich. (Mirror)


Meneja wa Manchester United Jose Mourinho alionekana kwenye mechi iliyomuhusisha Arnautovic, huku kukiwa na fununu kwamba anamtaka kikosini
Liverpool inataka kumuuza mshambuliaji wao Mfaransa Nabil Fekir mwenye umri wa miaka 24 kwa Lyon kwa euro milioni 60m (Le Parisien)
Na the Reds wanae mlindalango wa Barcelona Jasper Cillessen raia wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 29 kwenye orodha yake ya wachezaji wake. (Mundo Deportivo)
Bolt ajiandaa kukabili Mo Farah katika soka Old Trafford
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Italia Jorginho, mwenye umri wa miaka 26, yuko tayari kujiunga na kikosi cha Manchester City kutoka Napoli baada ya kununuliwa kwa euro milioni hamsini 50m baaada ya kukubali mkataba wa miaka mitano na Man city .

BBC: Sources

No comments:

Post a Comment