TUMUSIFU BWANA

prop

Friday 27 April 2018

TETESI ZA SOKA BALANI ULAYA IJUMAA YA 27.2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa anahitaji sifa kwa kumleta Chelsea mshambuliaji wa Misri mwenye umri wa 25 Mohamed Salah wakati alipokuwa mkufunzi wa Chelsea na sio lawama ya kumuuza mchezaji huyo katika klabu ya Roma 2016. (ESPN)
Tottenham iko tayari kumuuza beki wake wa kushoto Danny Rose, 27, beki wa kati wa ubelgiji Toby Alderweireld, kiungo wa kati wa Kenya Victor Wanyama, 26, na kiungo wa kati wa Ubelgiji Mousa Dembele kuchangisha £170m huku mkufunzi Mauricio Pochettino

Danny Rose
Mkufunzi wa Leicester City Claude Puel anapigania kuokoa kazi yake katika klabu hiyo huku timu hiyo ikipanga kufanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake mwisho wa msimu huu..
Mshambuliaji wa Wales Gareth Bale amekasirishwa na hatua ya klabu hiyo kutomchezesha mara kwa mara lakini kuna wasiwasi wa iwapo kuna klabu ya Uingereza itakayoweza kumnunua mchezaji huyo. (Guardian)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption
Gareth Bale
Arsenal itashindana na Atletico Madrid na Napoli katika kumwania kipa wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Bernd Leno, ambaye anapatikana kwa dau la £17.5m. (Bild via Sun)
West Ham wamejiunga katika mbio za kumsajili beki wa Ireland Kaskazini Jonny Evans kwa dau la £3m huku timu hiyo ya ligi ya Premia ikijiandaa na kushushwa daraja kwa West Brom(Mirror)

No comments:

Post a Comment