TUMUSIFU BWANA

prop

Monday 16 April 2018

Tazama magori ya simba vs prisons 2_0 kipindi cha kwanza

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Matokeo Simba vs Prisons VPL 16 April 2018

Matokeo Ya Mchezo kati ya Simba dhidi Ya Tanzania Prisons mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara Vodacom Premier League uwanja wa Taifa Jijini Dar Es Salaam.

>> Soma habari za Simba Hapa <<

Timu ndiyo zinaingia uwanjani zikitokea Vyumbani, Simba wamevaa tshirts nyekundu na Bukta zao ni Nyeupe.

Wakati Prisons wamevaa Kijani Tshirts na Bukta za Kijani Pia

Mwamuzi wa kati ni Shomari Lawi kutoka Mwanga Kigoma.

Tayari timu zote zipo kwenye Uwanja na Muda wowote mechi Itaanza

Mechi Imeanza katika uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam

Dakika ya kwanza SImba wanapata Kona

Kona inashindwa kuwa na madhara yoyote Langoni mwa Tanzania Prisons Kipa Aron Anadaka

Dakika ya 4 Timu zinacheza kwa Kusomana matokeo yakiwa bado ni tasa

Dakika ya 7 Mohammed Rashid alijaribu kuchomoka lakini akawekwa chini na Juuko Murshid, Inapigwa Faulo mabeki wa Simba wanaondoa mpira kwenye hatari

Dakika 10

Simba 0 – 0 Prisons

Dakika ya 11 Simba wanapata Kona, Inapigwa na Shomari Kapombe lakini Kipa wa Prisons anadaka mpira Huo

Dakika 15

Simba 0 – 0 Tanzania Prisons

Dakika ya 17 Simba wanapata Kona ya Tatu

Kona inapigwa na Kichuya mabeki wanaokoa na Kuondoa mpira kwenye eneo la hatari, Bado 0 kwa 0

Dakika ya 20 Offside John Bocco mara baada ya Kupenyezewa mpira na Shiza Kichuya

Dakika ya 22 Simba wawanapata Kona ya 4 lakini haina madhara kwa Prisons.

Simba wanapata tena Kona Hii ni ya Tano matokeo yakiwa 0 kwa 0

Dakika ya 23 Eliuta Mpepo anajaribu kupiga Shuti linaenda pembeni ya Lango la Simba

Dakika ya 27 Mpira Unachezwa zaidi katikati ya Uwanja wanachofanya walinzi wa Prisons ni kutibua Mipira Ya Simba huku wao wakitegemea kucheza mipira Mirefu

Dakika ya 32 Shomari Kapombe anamimina Krosi safi beki wa Prisons anatoa inakuwa kona ya 6 kwa Simba.

Inapigwa Kona inatoka Nje.

Simba 0 – – Prisons

Simba wanapata Kona Mbili mfululizo, Wanakuwa na Kona nane mpaka sasa Prisons hawana kona hata Moja

Goaaaaaaaaaaal dakika ya 35 Nahodha John Bocco anaipatia Simba bao la Kuongoza.

Ulipigwa Mpira na Erasto Nyoni kutokea Pembeni ikaenda ikagonga mwamba wa pembeni ukarudi uwanjani na Bocco akapigwa Kichwa Kikazama golini.

Dakika 40

Simba 1 – 0 Bocco

No comments:

Post a Comment