TUMUSIFU BWANA

prop

Tuesday 24 April 2018

ENDELEZA SIMULIZI YA BINTI ALIYE FUFUKA

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.

IJUMAA…Soma mwanzo wa hadithi>>>>
“Kwa vile mama yako ndiye amesema hivyo, nitafanya bidii nipate hizo pesa kabla ya wiki hii kumalizika.”
“Itakuwa vyema kama zitapatikana haraka.”

SASA ENDELEA…
“INA maana kwamba Alhakim akirudishiwa hizo pesa na uchumba utakuwa umekwisha?”
“Sasa nani atamkubali mchumba aliyetiwa mimba na mtu mwingine?”
“Kwa hiyo mimi ndiye nitakuwa mchumba wako?”
“Si unafahamu mila zetu, wewe ndiye umeniharibu na ndiye utakayenioa.”
“Baba anafahamu hivyo?”
“Baba hafahamu chochote. Mama ndiye niliyezungumza naye. Sasa labda yeye atamwambia.”
“Kwa hayo mawazo kwamba nirudishe hizo pesa za Alhakim yametoka kwa mama?”
“Yametoka kwa mama. Ameona mambo yameshaharibika sasa anataka kuyaweka sawa. Alihisi tatizo kubwa ni pesa za watu.”

“Ni lazima tufahamu na mawazo ya baba, ni kama hayo ya mama au atakuwa na mawazo mengine.”
“Mshauri wa baba ni mama. Kama mama amesema hivyo, baba hatakuwa na kipingamizi. Watazungumza wenyewe.”
“Sasa mimi nitahangaikia hizo pesa. Kwa upande wangu pia sipendi yatokee matatizo kwa Alhakim.”
“Nitakwenda kumueleza mama ulivyoniambia.”
Kidogo nilimuona Macheo akiwa amepata ahueni. Na kutokana na maelezo ya Macheo, mimi pia nilipata ahueni.

Sote wawili tukahisi furaha ndani ya mioyo yetu. Tulikuwa kama tumeutua mzigo mzito uliokuwa unatuelemea.
Niliporudi nyumbani nikamueleza mama tulivyozungumza na Macheo.
“Sasa hizo pesa atazileta lini?” Mama akaniuliza.
“Ameniambia wiki hii.”
“Itabidi azilete yeye mwenyewe ili tuweze kumtambua.”
“Nitamwambia azilete mwenyewe. Kwani umeshamwambia baba?”

“Nilikuwa ninasubiri maelezo kutoka kwa huyo mwanaume. Sasa kama amesema atatoa hizo pesa, nitakuwa nimeshapata maelezo ya kumwambia baba yako ingawa ninafahamu kwamba atakasirika sana kwa sababu umeharibu heshima yake kwa Alhakim.” Hapo sikusema kitu. Nilinyamaza kimya.“Sasa utamueleza lini baba?”“Nitamueleza leo.”“Sasa akiniita nitamwabia nini?”“Swali hilo unamuuliza nani? Kwani mimi umenieleza nini?”“Wewe ni mama, yule ni baba. Si umesema ukimwambia atakasirika!” “Kama atakasirika utafanya nini na kosa limeshatokea?” “Basi akiniita na wewe uwe hapohapo.”
Mama hakukubali wala kukataa, nilipomwambia hivyo aliinuka na kwenda uani kuendelea na shughuli zake. Nikabaki peke yangu nikiwaza.

Nilikuwa ninamuonea haya sana baba kuliko mama. Akiambiwa ile habari na akifahamu nina mimba, kwa kweli nitamkwepa. Sitaweza kuusogeza uso wangu mbele yake.
Mzee yule mawazo yake yote yalikuwa kwa Alhakim. Kitendo cha Alhakim, mtu mwenye pesa zake, kunitaka mimi si tu kilimpa matumaini ya maisha baba yangu, bali kilimtia fahari kuona kwamba mwanawe ataolewa na mtu mwenye pesa.
Nilikuwa ninafahamu kwamba siku zote baba yangu alikuwa akiombea nimalize masomo ili niolewe na Alhakim. Sasa akisikia nimepata mimba, sikuweza kuelewa atafedheheka kiasi gani.
Lakini tatizo ndiyo limeshatokea. Tangu hapo Alhakim sikumpenda licha ya kuwa na pesa. Niliyekuwa nikimpenda ni Macheo ambaye nilianzana naye tangu nikiwa kidato cha tatu.

Lakini nguvu ya wazazi wangu ndiyo iliyonifanya nimkubali Alhakim licha ya kuwa mtu mzima kama baba yangu. Sikupanga nifanye ufisadi wowote wala Macheo hakupanga hivyo. Kilichotokea kilikuwa ni bahati mbaya. Sikupenda kitokee.
Siku ile ambayo mama aliniambia atazungumza na baba, asubuhi yake baada ya kunywa chai, baba akaniita sebuleni. Moyo wangu ulishtuka sana. Nilishafahamu nilichokuwa ninaitiwa. Nikaenda sebuleni kumsikiliza.
“Kaa hapo,” akaniambia.

Uso wake na sauti yake viliniashiria kuwa alikuwa amechukizwa.
Baada ya kukaa, akaniambia.
“Mwanangu kwa nini unanifanya hivi?”
Ili kukwepa macho yake makali yaliyokuwa yakinitazama, niligeuza uso wangu upande mwingine.
“Kama ulikuwa humtaki huyu mchumba ungesema kuliko kunifedhehesha kiasi hiki!” Baba aliendelea kuunguruma. Mama hakuwepo. Moyoni mwangu nilikuwa ninamuita mama awepo pale ili amtulize baba.

“Mama uko wapi?” Nilikuwa nikisema peke yangu.
“Sasa mimi nitamwambia nini Saidi Omar (Alhakim) wakati ameshatoa pesa zake kwa sababu yako?”
“Pesa zitatole

No comments:

Post a Comment