TUMUSIFU BWANA

prop

Friday 30 March 2018

Yanga ya kanusha kumuhitaji mudathir yahya

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Mudathir Yahya anazidi kutawala kwenye vichwa vya habari za michezo akihusishwa kujiunga na Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa taji la VPL.

Kiungo huyo anaecheza kwa mkopo Singida United amemaliza mkataba wake na klabu ya Azam hivyo kwa sasa ni mchezaji huru na anaweza kujiunga na timu yoyote atakayoamua mwenyewe.

Mara baada ya uongozi wa Azam kupitia msemaji wake Jafar Idd kutangaza kumruhusu mudathir kuendelea na maisha yake ya soke sehemu nyingine, Yanga inatajwa kuanza kuiwinda saini ya mchezaji huyo wa Zanzibar Heroes na Taifa Stars.

Mwenyekiti wa kamati ya mashindano Yanga Hussein Nyika amesema hadi sasa klabu yao haijaongea na mchezaji yeyote wala hawajafanya usaji wa aina yoyote.

“Hakuna kitu kama hicho sisi (Yanga) tunaelekeza nguvu zetu kwenye mashindano, hatujafika kipindi cha usajili. Yanga inafanya usajili kwa taratibu zake, baada ya mashindano kumalizika lazima mwalimu atuletee ripoti yake anahitaji maeneo gani yajazilizwe hapo ndipo tutaingia msituni kwa ajili ya usajili.”

“Hadi sasa hivi hatujaongea na mchezaji wa aina yoyote na hatujafanya usajili wa aina yoyote. Hatuwezi kufanya usajili kwa sababu mchezaji yupo huru, usajili wetu huwa tunafanya baada ya kupokea ripoti ya mwalimu na mapendekezo yake. Mwalimu ndio anafanya usajili sisi tunatekeleza ambayo mwalimu anaagiza.”

Uongozi wa Singida United umesema, pamoja na Mudathir Yahya kumaliza mkataba na Azam wao wana mipango nae na huenda wakaingia mkataba wa muda mrefu na mchezaji huyo

No comments:

Post a Comment