Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
SALUM MKEMI ATANGAZA KUJIUZULU UONGOZI YANGA
Mjumbe wa Kamati wa Utendaji ya Yanga, Salum Mkemi.
MJUMBE wa Kamati wa Utendaji ya Yanga, Salum Mkemi amejiuzulu nafasi uongozi ndani ya klabu hiyo kuanzia leo. Maneno hayo ameyasema kupitia akaunti yake ya Instagram baada ya timu ya Yanga kuaga kwenye michuano ya Sportpesa Super Cup inayoendelea nchini Kenya baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Kakamega Boys kwenye mchezo uliopigwa kwenye Dimba la Ifraha nchini Kenya.
Haya ndo maneno aliyoyasema kupitia akaunti yake ya Instagram
Kusema Kweli Viongozi Hatukwepi Lawama Hizi
Kwa Hakika Tumepata Aibu Kubwa Nikiwa kama Kiongozi napaswa kuwajibika kwa Hili
Ni hatua nzuri ya kupisha Mawazo mapya kwa Wanachama wengine kuongoza Timu na Kutupeleka Mbele, pia ningependa kuwashauri Viongozi wenzangu wajitathimini na ikibidi nao waachie Ngazi Ufanye Uchaguzi Mkuu kwa Pamoja tupate Viongozi wapya kabla msimu Mpya Haujaanza
Napenda kuomba samahani kwa wote niliowakwaza na nimesamehe wote walio nikikwaza.
Naomba kutamka Rasmi Mimi Salum Mkemi
Nijaizulu nafasi zangu zote za Uongozi ndani ya Klabu yangu pendwa Young Africans Sports Club “YANGA ” kuanzia tarehe ya Leo 03/06/2018
Nawatakia kila la kheri Viongozi wenzangu waliobaki na Kuwataka Radhi tena Wanachama, Wapenzi na Mashabiki wa Yanga kwa Matokeo mabovu tuliyopata naomba tusamehane.
Nawashukuru kwa Muda mlionipa kuiongoza Klabu hii kubwa Afrika
Naomba Kuwajibika kwa Kujiuzulu
Wenu Mwanachama Mwenzenu Mtiifu
SALUM MKEMI
NIMENG’ATUKA
prop
Sunday, 3 June 2018
SALUM MKEMI ATANGAZA KUJIUZULU UONGOZI YANGA
Recommended Articles
- Michezo
Julio: Alikiba Anaweza Kucheza hata Ulaya Jun 10, 2018
KOCHA wa Dodoma FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ameweka wazi kuwa msanii wa Bongo Fleva nchini, Ally Salehe Kiba ‘Alikiba’...
- Michezo
MAMBO MATANO MAKUBWA WALIO HAFIKIANA YANGA SC MKUTANO MKUUJun 10, 2018
Club ya Dar es Salaam Young Africans leo Jumapili ya June 10 2018 ilifanya mkutano mkuu na wanachama wake katika ukumbi wa Police Officers Mess M...
- Michezo
GOR MAHIA WAIPA KICHAPO SIMBA SC...SAFARI YA ULAYA NDO BASI TENAJun 10, 2018
Moja kati ya siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka Bongo ni leo June 10 2018, kwani ndio ilikuwa siku inayochezwa mchezo wa...
- Michezo
MATOKEO GOR MAHIA VS SIMBA SC 2_0 KIPINDI CHAPILIJun 10, 2018
Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 June 2018 Sportpesa Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 June 2018 Sportpesa Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 Ju...
Newer Article
KURASA ZA MAGAZETI MBALIMBALI JUMATATU YA 4.2018
Older Article
BODI YA MIKOPO YASITISHA MIKOPO KWA WANAFUNZI WA DIPLOMA
Labels:
Michezo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment