Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Arsenal wameimarisha ofa yao kwa kiungo wa kati Jack Wilshere. Mkataba wa mchezaji huyo wa miaka 26 unafikia kikomo mwisho wa msimu na amekuwa akitafutwa na Wolves na Everton. (Mirror)
Mchezaji anayesakwa sana na Liverpool Max Meyer hatachezea tena Schalke baada yake kufukuzwa kutoka mazoezini na kutoka kwenye kikosi cha kwanza. Meyer, mshambuliaji mwenye miaka 22, aliadhibiwa baada yake kumkosoa mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo ya Bundesliga Christian Heidel. (Sky Sports)
Jedwali la Msimamo wa ligi ya EPL 2017/18
Rais wa Real Madrid Florentino Perez amesema Gareth Bale, 28, anataka kusalia Bernabeu licha ya tetesi kwamba huenda mshambuliaji huyo wa Wales akahama. (Sun)
Pep Guardiola amesema uamuzi ufaao utafanywa kuhusu kipa wa Manchester City Joe Hart iwapo West Ham wataamua kutobadilisha mkataba wake wa sasa wa mkopo kuwa uhamisho wa kudumu. (Mirror)
Marouane Fellaini, 30, anataka Manchester United wampe mkataba wa muda mrefu zaidi kushinda mwaka mmoja ambao wamemuahidi kwa sasa Old Trafford. (ESPN)
Haki miliki ya pichaHUW EVANS PICTURE AGENCY
Kiungo wa kati wa Arsenal Santi Cazorla anatumai kwamba ataweza kurejea kucheza kabla ya mwisho wa msimu. Mhispania huyo mwenye miaka 33 hajachezea Gunners tangu mwaka 2016 kutokana na jeraha la mguuni ambalo limekosa kupona. (AS)
Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 30.04.2018
Meneja wa Shakhtar Donetsk Paulo Fonseca amekataa ofas kutoka kwa Everton baada ya kuanza kuangazia kumrithi Arsene Wenger Arsenal, kwa mujibu wa mwanahabari Guillem Balague. (Express)
Thierry Henry na Tony Adams ni miongoni mwa watu mashuhuri 100 wa Arsenal ambao wamealikwa kwa mechi ya mwisho ya Wenger nyumbani, ambapo watasherehekea miaka 22 ya Mfaransa huyo katika klabu hiyo. (Mail)
Mshambuliaji wa West Ham Andy Carroll, 29, alifukuzwa kutoka mazoezini Jumatatu na meneja wa klabu hiyo David Moyes baada ya wawili hao kukorofishana. Klabu hiyo inatarajiwa kuanza uchunguzi kuhusu kisa hicho. (Telegraph)
prop
Tuesday, 1 May 2018
TETESI ZA SOKA BALANI ULAYA JUMANNE YA 1.05.2018
Recommended Articles
- Michezo
Julio: Alikiba Anaweza Kucheza hata Ulaya Jun 10, 2018
KOCHA wa Dodoma FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ameweka wazi kuwa msaÂnii wa Bongo Fleva nchini, Ally Salehe Kiba ‘Alikiba’...
- Michezo
MAMBO MATANO MAKUBWA WALIO HAFIKIANA YANGA SC MKUTANO MKUUJun 10, 2018
Club ya Dar es Salaam Young Africans leo Jumapili ya June 10 2018 ilifanya mkutano mkuu na wanachama wake katika ukumbi wa Police Officers Mess M...
- Michezo
GOR MAHIA WAIPA KICHAPO SIMBA SC...SAFARI YA ULAYA NDO BASI TENAJun 10, 2018
Moja kati ya siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka Bongo ni leo June 10 2018, kwani ndio ilikuwa siku inayochezwa mchezo wa...
- Michezo
MATOKEO GOR MAHIA VS SIMBA SC 2_0 KIPINDI CHAPILIJun 10, 2018
Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 June 2018 Sportpesa Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 June 2018 Sportpesa Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 Ju...
Labels:
Michezo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment