TUMUSIFU BWANA

prop

Tuesday 27 March 2018

Tetesi za usajili barani ulaya jumanne ya 27 march

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Barcelona wanapanga kuwasilisha ombi la kutaka kumchukua beki wa Manchester United Luke Shaw mwisho wa msimu. Beki huyo wa kushoro wa miaka 22 kutoka England amekosolewa sana na meneja wa United Jose Mourinho wiki za karibuni. (Mirror)
Mabingwa wa Ufaransa Monaco ndiyo klabu ya karibuni zaidi kuonesha nia ya kumtaka kiungo wa kati wa Manchester United Marouane Fellaini. Mkataba wa mchezaji huyo wa miaka 30 kutoka Ubelgiji unamalizika mwisho wa msimu na anatarajiwa kuondoka Old Trafford. (Mail)
Dani Ceballos ambaye amekuwa akitafutwa na Liverpool ameambia anaweza kutoka Real Madrid mwisho wa msimu. Kiungo huyo wa kati Mhispania wa miaka 21 amekuwa pia anatafutwa na AC Milan na Juventus. (Mundo Deportivo kupitia Talksport)
Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu

No comments:

Post a Comment