TUMUSIFU BWANA

prop

Tuesday 27 March 2018

Brazil wataweza kulipa 7_1 Leo ?

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Mkufunzi wa Brazil Tite amesema timu yake bado inatatizwa na "mizimu" ya kipigo cha 7-1 ambacho walipokezwa na Ujerumani katika nusu fainali ya Kombe la Dunia miaka minne iliyopita.
Mataifa hayo mawili yatakutana tena wka mara ya kwanza Jumanne mjini Berlin tangu Brazil walipoaibishwa kwao nyumbani wakati wa michuano hiyo ya Kombe la Dunia.
"Hii ina maana kubwa sana kisaikolojia - hakuna anayehitaji kujidanganya kuhusu hilo," Titea aliambia jarida la Kicker.
"Matokeo hayo ya 7-1 ni kama mizimu, watu bado huyazungumzia. Kadiri unavyoyazungumzia zaidi, ndivyo mizimu hii inavyochukua muda mrefu kutoweka."
Brazil yafuzu Kombe la Dunia 2018
Shujaa wa Panama anayepanga kuhangaisha England Kombe la Dunia
Toni Kroos alifunga mabao mawili wakati huo naye Miroslav Klose akavunja rekodi ya ufungaji mabao Kombe la Dunia mwaka 2014 Ujerumani walipoafanikiwa kujiweka mbele 5-0 dakika 29 za kwanza kwenye nusu fainali hiyo.
Katika mechi hiyo ya kimataifa ya kirafiki itakayochezewa Berlin, kiungo wa kati wa Manchester City Fernandinho anatarajiwa kuingia uwanjani nafasi ya Douglas Costa.
Hilo litakuwa ndilo badiliko pekee kwenye timu ambayo ililaza Urusi 3-0 mjini Moscow mnamo Ijumaa bila nyota wao Neymar ambaye anauguza jeraha.

No comments:

Post a Comment