TUMUSIFU BWANA

prop

Monday 30 April 2018

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA JUMATATU YA 30.2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Mkufunzi mkuu wa Real Madrid Zinedine Zidane amesema washambuliaji wake Gareth Bale, 28, na Karim Benzema, 30, "watasalia" katika klabu hiyo licha ya tetesi kudokeza kwamba huenda wakahama. (Star)
Bournemouth wanaaminika kuwa tayari kushindana na Tottenham na Manchester United katika kutafuta saini ya beki wa Celtic kutoka Scotland Kieran Tierney, 20. (Sun)
Meneja wa Arsenal anayeondoka Arsene Wenger atachukua "miezi minne hadi mitano" kuamua kuhusu mustakabali wake. (London Evening Standard)
Wakufunzi wanaopigiwa upatu kumrithi Arsene Wenger
Mshambuliaji wa zamani wa Celtic Chris Sutton anasema "litakuwa jambo zuri sana kwa soka ya Scotland iwapo Steven Gerrard atakuwa meneja wa Rangers". Hata hivyo amemtahadharisha nahodha huyo wa zamani wa Liverpool kwamba "hatua kama hiyo inaweza kufuta matumaini yake ya kuwa mkufunzi tajika hata kabla yake kuanza" (Mail)
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino amekataa kuthibitisha iwapo atakuwa kwenye klabu hiyo msimu ujao. (Mirror)
Haki miliki ya pichaBBC SPORT
Naye meneja msaidizi wa Liverpool Zeljko Buvac ameihama klabu hiyo baada ya kuzozana na meneja wa sasa Jurgen Klopp. (Daily Record)
Mshambuliaji wa Crystal Palace mwenye miaka 27 Christian Benteke, ambaye amesalia na miaka miwili pekee katika mkataba wake na klabu hiyo, amesema atajadiliana kuhusu hatima yake na klabu hiyo mwisho wa msimu. (Mail)
Mfanyabiashara Mmarekani Shahid Khan anaweza akaukubali mpangilio wa "lipia ukiendelea kuchezea" kati yake na Chama cha Soka cha England kama sehemu ya makubaliano kati yake na chama hicho kuhusu ununuzi wa uwanja wa Wembley. Mpangilio kama huu unaweza kuifanya nafuu kwa FA kutumia viwanja vya nje kucheza mechi zake. (Times )
Klabu ya West Brom ambayo imo hatarini ya kushushwa daraja itapigania kusalia na beki wa England Craig Dawson mwenye miaka 27 ambaye anatafutwa na Burnley, Wolves na West Ham. (Mirror)

No comments:

Post a Comment