Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
ULIMWENGU AREJEA AFRIKA NA KUJIUNGA NA WAKONGWE WA SUDAN
Mshambuliaji Thomas Ulimwengu ameamua kurejea barani Afrika na kujiunga na klabu kongwe ya Sudan ya Al Hilal.
Ulimwengu ambaye hucheza nafasi ya ushambuliaji na wakati mwingine winga, nafasi hizo zote ndani ya timu hiyo zina watu wa maana ambapo mmoja anatoka Nigeria na mwingine Brazil.
Mbrazili, Geovane Maranhao, anacheza namba tisa kwenye kikosi hicho, huku Mnigeria, Azeez Shobola akicheza winga, hivyo Ulimwengu anatakiwa kufanya juhudi kubwa kuhakikisha anakuwepo kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Meneja wa Ulimwengu, Jamal Kisongo, alisema kuwa tayari mchezaji huyo amepata timu lakini hawezi kuweka wazi mpaka pale vibali vitakapokamilika.
Straika huyo tayari anaonekana katika mtandao wa Transfer Market, ambao unaonyesha kuwa amesajiliwa na klabu ya Al Hilal, ingawa thamani yake imeshuka tofauti na alivyokuwa na TP Mazembe.
Ulimwengu mara ya mwisho alisajiliwa na klabu ya AFC Eskilstuna ya Sweden akitokea kwenye klabu ya TP Mazembe ya Congo, lakini alishindwa kucheza kutokana na kuandamwa na majeraha ya goti ambayo yamemuweka nje kwa muda mrefu.
Hata hivyo ikiwa inaaminika kuwa alisaini wikiendi iliyopita, Championi jana lilimtafuta Ulimwengu kwa muda mrefu lakini hakupatikana, juhudi zinaendelea.
prop
Thursday, 24 May 2018
ULUMWENGU ALA DILI MIAKA LA USAJILI BALANI AFRIKA IJUMAA YA 25.2018
Recommended Articles
- Michezo
Julio: Alikiba Anaweza Kucheza hata Ulaya Jun 10, 2018
KOCHA wa Dodoma FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ameweka wazi kuwa msaÂnii wa Bongo Fleva nchini, Ally Salehe Kiba ‘Alikiba’...
- Michezo
MAMBO MATANO MAKUBWA WALIO HAFIKIANA YANGA SC MKUTANO MKUUJun 10, 2018
Club ya Dar es Salaam Young Africans leo Jumapili ya June 10 2018 ilifanya mkutano mkuu na wanachama wake katika ukumbi wa Police Officers Mess M...
- Michezo
GOR MAHIA WAIPA KICHAPO SIMBA SC...SAFARI YA ULAYA NDO BASI TENAJun 10, 2018
Moja kati ya siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka Bongo ni leo June 10 2018, kwani ndio ilikuwa siku inayochezwa mchezo wa...
- Michezo
MATOKEO GOR MAHIA VS SIMBA SC 2_0 KIPINDI CHAPILIJun 10, 2018
Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 June 2018 Sportpesa Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 June 2018 Sportpesa Matokeo Gor Mahia vs Simba leo 10 Ju...
Newer Article
HABALI NJEMA KUTOKA 1XBET IJUMAA YA LEO
Older Article
DONDOI ZA MAGAZETI YA MICHEZO,UDAKU NA BURUDANI YA IJUMAA YA TAREE 25.2018
Labels:
Michezo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment