TUMUSIFU BWANA

prop

Wednesday 16 May 2018

PEP GUARDIOLA KUSHINDA TUNZO YA KOCHA BORA WA LIGI KUU YA ENGLAND

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Pep Guardiola ameshinda tuzo ya Kocha Bora wa Ligi Kuu England kufuatia kuiwezesha Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu nchini humo.

Guardiola ameisaidia City kufikisha pointi 100 msimu huu pamoja na kushinda jumla ya mechi 32 huku akipoteza michezo miwili pekee.

Mbali na ushindi huo, kikosi chake kimeweza kufunga jumla ya mabao 106 na kikiweza kwenda sare katika michezo minne.

Guardiola alijiunga na Manchester City msimu wa 2016/17 akitokea Bayern Munich inayoshiriki ligi ya Bundesliga.

No comments:

Post a Comment