TUMUSIFU BWANA

prop

Wednesday 2 May 2018

Kwani kusoma nikujua kingereza ? Rais ahoji

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli amehoji wanafunzi wa chuo cha Mkwawa kwamba kujua kusoma ni kujua Kiingereza.



Rais Magufuli ameyasema hayo leo, Mei 2 wakati akizungumza na wanafunzi pamoja na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa, kilichopo mkoani Iringa wakati akitoa ufafanuzi wa shule za private na shule za Sekondari.

“Eti mtu amemaliza form 4 hajui kuandika barua ya kingereza. Kwani kusoma ni kujua kingereza? Wachina wanajua kingereza? mbona wanatengeneza mashine,” amehoji Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amesema kuwa “Shule za private wanafunzi wake wanachujwa, wakifika form 2 kuingia form 3 wanawachuja tena. Wanabaki na ile cream ili waonekane wanaongoza. Serikali inayowapenda wananchi wake haiwezi ikafanya hivyo.”

No comments:

Post a Comment