TUMUSIFU BWANA

prop

Tuesday 22 May 2018

Harry Kane apewa kitambaa cha unahodha england

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
HARRY KANE APEWA KITAMBAA CHA UNAHODHA ENGLAND KWA KAZI MAALUM RUSSIA



Mshambuliaji wa Tottenham Hotspurs, Harry Kane, ametangazwa kuwa Nahodha wa kikosi cha timu ya Taifa ya England kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia huko Urusi mwaka huu.

Kane ameteuliwa na Kocha Gareth Southgate kuchukua nafasi hiyo baada ya kuonesha mchango mkubwa katika klabu yake msimu huu.

Southgate amemteua Kane zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi mapema mwezi ujao.

Nahodha wa Liverpool, Jordan Henderson pamoja na kiungo wa Tottenham, Eric Dier waliwahi kuwa manahodha wa kikosi cha England chini ya Southgate lakini awamu hii chaguo limemdondokea Kane.

No comments:

Post a Comment