TUMUSIFU BWANA

prop

Saturday 28 April 2018

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA JUMAMOSI YA 28/2018

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Jana Ijumaa ya April 27 2018 kiungo wa FC Barcelona Andres Iniesta alitangaza rasmi mbele ya waandishi wa habari kuwa anaondoka timu hiyo, moja kati ya watu ambao wamechukua headlines ni Lionel Messi kutoonekana wakati Andres Iniesta anaaga, hivyo imezua maswali mengi kutokana na wawili hao wamecheza kwa pamoja muda mrefu.

Leo imegundulika sababu ya Lionel Messi kutokuwepo wakati Iniesta anaaga ni kutokana na yeye na familia yaku kuwa busy na kushughulikia passport zao mpya, hivyo alikuwa hana budi kuikosa siku ya Iniesta ambaye ameaga kuwa msimu huu ndio mwisho kuichezea FC Barcelona na ataondoka.



Lionel Messi ambaye ni mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or mara tano kwa pamoja yeye na Andres Iniesta wamecheza FC Barcelona toka 2004 Messi akiwa na umri wa miaka 17 na Iniesta akiwa na umri wa miaka 20, Iniesta anaondoka FC Barcelona na amesema kuwa anaenda kucheza nje ya bara la Ulaya kutokana na kuwa hahitaji kucheza dhidi ya FC Barcelona.
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amepewa fursa kuwa mkufunzi tajiri zaidi duniani iwapo atajiunga na ligi kuu ya China.(Mirror)
Wenger ameombwa kuchukua wadhfa wa meneja mkuu katika klabu ya PSG(Le10 via Talksport)
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa kipa David de Gea hataondoka katika klabu hiyo mwisho wa msimu huu.
Arsene Wenger: Nililazimishwa anasema kuwa ameanza mazungumzo na klabu hiyo kuhusu hatma yake ya siku zijazo. Amehusishwa na Barcelona na Manchester United (Sun)
Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola yuko tayari kumzuia Mikel Arteta kusalia miongoni mwa makocha wake licha ya raia huyo wa Uhispania kuhusishwa na Arsenal. (Mirror)
Mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte huenda akakosa wadfha wa ukufuzi wa timu ya taifa ya Itali. Conte mwenye umri wa miaka 48 anataka mkataba mpya wa miaka mitano lakini shirikisho la soka nchini Itali limekataa kuafiia mahitaji hayo.(Times - subscription only)

No comments:

Post a Comment