TUMUSIFU BWANA

prop

Sunday 25 March 2018

Rais wa afrika anaye ongoza kutoka nje ya inchi yake

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Rais wa Cameroon Paul Biya amekuwa madarakani kwa takriban miaka 35. Lakini utawala wake wa miaka mingi umekuwa gumzo nyumbani , muda anaotumia akiwa katika mataifa ya kigeni umezua hisia za kimataifa.
Akikosolewa na wengine kutokana na uongozi wake wa kuwa nje ya taifa , rais Paul Biya wa Cameroon hivi karibuni aliitisha mkutano wa baraza lake la mawaziri kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka miwili.
Uchaguzi wa urais hufanyika mwezi Oktoba na raia wa Cameroon husubiri kusikiza iwapo rais huyo mwenye umri wa miaka 85 atawania muhula mwengine.
MATANGAZO

Lakini hakuna tangazo kama hilo lililofanywa katika mkutano huo. Bwana Biya amekuwa uongozini tangu 1982, akiwa ni miongoni mwa viongozi wa bara Afrika walioongoza
Chini ya uongozi wake Cameroon imenusurika mgogoro wa kiuchumi kabla ya kubadilika kutoka kuwa taifa la chama kimoja hadi kuwa na vyama vingi.
Lakini pia taifa hilo limekumbwa na ufisadi wa kiwango cha juu mbali na kuzorota kwa uhuru wa kidemokrasia uliopatikana na kufutiliwa mbali kwa muda wa kipindi cha rais mwaka 2008 ambao ulimruhusu mzee huyo kuwania tena urais mwaka 2011.
Haki miliki ya pichaAFP
Image caption
Rais Biya amekuwa nchini China wiki hii
Bara la Afrika la leo linabadilika .Kipindi cha viongozi walioongoza bara hilo kwa miongo kadhaa kinaendelea kuyoyoma .
Runinga zinazotumia setlaiti na mtandao umekuwa ukiwaelezea raia mabadiliko ya kidemokrasi katika mataifa mengine ya jangwa la Sahara.
Asilimia 60 ya raia wa Cameroon wako chini ya umri wa miaka 25 na hawakuwa wamezaliwa wakati Paul Biya alipochukua madaraka.
Kuna shinikizo kuu ya ajira na maisha mazuri. Chama cha upinzani cha Social Democratic Front sasa kimetambua ukweli huo.
Mapema mwaka huu kiongozi wa chama hicho John Fru Ndi, 76 alijiondoa na kumwachia mgombea mpya mfanyibiashara mwenye umri wa miaka 49 na rubani wa zamani Joshua Osih.
Hoteli ya Uswizi
Hii ndio changomoto inayomkumba bwana Biya huku akiamua iwapo atasimama kwa awamu nyengine ambayo itamfanya kuongoza muhula mwengine wa nne madarakani katika taifa ambalo linataka mabadiliko.
Kutokuwepo kwake katika taifa hilo kumewafanya wakosoaji wake kutoa hisia kali dhidi yake.
Safari zake za kigeni zimesababisha makabiliano ya mtandaoni kati ya gazeti la Tribune na mradi wa uhalifu unaopangwa na Ufisadi OCCRP ambao ulihesabu muda unaotumiwa na rais huyo ugenini kwa kutumia ripoti za magazeti ya kila siku.
Mradi huo wa kukabiliana na ufisadi na ripoti za uhalifu unakadiria kwamba rais alitumia takriban siku 60 nje ya taifa hilo mwaka uliopita katika ziara za kibinafsi.
Pia imedaiwa kwamba alitumia thuluthi moja ya mwaka 2006 na 2009 ughaibuni.
Hoteli ya Intercontinental mjini Geneva ndio imedaiwa kuwa anayoipenda. Gazeti hilo linalomilikiwa na serikali lilitaja uchunguzi uliofanywa kuwa propanganda za uchaguzi.

No comments:

Post a Comment