TUMUSIFU BWANA

prop

Tuesday 27 March 2018

Fully time Tanzania vs DRC CONGO 2 _0

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
FULL TIME: MPIRA UMEMALIZIKA KUTOKA UWANJA WA TAIFA
Dak ya 94, Yahaya Zayd anaingia kuchukua nafasi ya Simon Msuva
Dak ya 93, Unapigwa huku, Stars wanaokoa
Dak ya 92, DRC wanajaribu kupenyeza kulia mwa Uwanja walau kupata bao la kufutia machozi, faulo, mpira unapigwa kuelekea Stars
Dak ya 91, Manula anapiga mbele huku kuwatafuta washambuliaji
DAKIKA 90 ZIMEMALIZIKA, ZIMEONGEZWA DAKIKA 4
Dak ya 89, Shomari Kapombe amebebwa kwenye machela kutolewa nje baada ya kuumia
Dak ya 87, Mabadiliko; Kichuya anatoka Uwanjani, nafasi yake inachukuliwa na Rashid Mandawa
Dak ya 86, Gooooooli, Kichuyaa, anafunga bao la pili kufuatia kazi nzuri aliyotengenezewa na Samatta
Dak ya 85, Zimesalia dakika 5 mpira kumalizika
Dak ya 84, Kadi ya njano anapewa beki wa FRC baada ya kumchezea madhambi Ibrahim Ajib
Dak ya 82, Gadieeeel, piga shuti moja lakini linapaa juu ya lango
Dak ya 82,  Mpira ni goli kiki, Kipa wa DRC anaanza upya
Dak ya 80, DRC wanapambana kupata bao hapa, Stars wanaondoka na mpira, kwake Samatta lakini DRC wanaokoa tena


Dak ya 79, Bado DRC wana mpira
Dak ya 78, Kwenda huku mbele sasa wachezaji wa DRC na mpira, wanajaribu kutafuta bao la kusawazisha
Dak ya 77, DRC wameshaanza, Stars wanaunyaka, piga huku mbele kwake Samatta tena, unamkuta Kichuyaaaaa, kipa anadaka, ilikuwa hatari
Dak ya 74, Goooooli, Mbwana Samatta anafunga bao la kwanza kwa njia ya kichwa kufuatia krosi nzuri ya guu la kushoto kutoka kwa Shiza Kichuya, Stars 1, DRC 0
Dak ya 73, Kocha Mayanga ameshindwa kukalia kiti chake, muda wote amesimama, hii ni kuhakikisha vijana wake wanapambana
Dak ya 71, Gadiel Michael anagangwa na madaktari baada ya kuumia mguu wakati akiokoa mpira uliokuwa unaelekea kwenye nyavu za Stars

Dak ya  70, Wachezaji wa akiba wa Stars wanapasha
Dak ya 68, Mpira umesimama, Banda amekaa chini
Dak ya 67, DRC na mpira, pigwa pasi moja, mabeki wa Stars wanaokoa na mpira unakwenda nje. Unarushwa huku, Manula anadaka
Dak ya 65, Kelvin Yondan anao mpira eneo la nyuma huku, pasia kwake Kichuya, DRC wanauchukua, hatarii huku langoni mwa Stars inatokea piga nikupige na DRC wanakosa goli la wazi kabisa, yangekuwa mambo mengine muda huu
Dak ya 64, DRC walishaanza, wanatoa nje, unarushwa kuelekea langoni kwao
Dak ya 63, Bahati mbaya inaiandama Stars, Msuva anakosa kuiandika tena Stars bao, mpira unamtoka miguuni na kwenda nje, Goli Kiki
Dak ya 62, Offside, Stars wanaotoea, bado matokeo ni 0-0
Dak ya 61, Ajib anashindwa kutumia nafasi yake ya kwanza vizuri, baada ya kupiga shuti na kwenda nje ya goli
Dak ya 60, Mpira ni goli kiki, unapigwa kuelekea DRC, Manula anaanza taratibu na Yondan, pigwa mbele huku

Dak ya 59, Mohammed Issa anatoka baada ya kuumia, Ibrahim Ajib anachukua nafasi yake
Dak ya 58, DRC wako langoni mwa Stars, wanafanya jitihada za kuandika bao la kwanza, mpira unakuwa faulo, unapigwa kuelekezwa DRC
Dak ya 57, Mohammed Issa ameumia, mpira umesimama kwa muda
Dak ya 57, Goli Kiki, wakati huo Manula anawaonya wachezaji wake wazidi kuwakaba DRC, wasiwaachie
Dak ya 56, Stars wanaanza tena eneo la ulinzi, pigwa kwake Msuva huku mbele, mabeki wa DRC wanakuwa maridadi wanacheza kuokoa mpira
Dak ya 54, Ndombe anatoka upande wa DRC, nafasi yake inachukuliwa na Junior Kabananga
Dak ya 54, DRC wanakosa nafasi ya kupata bao la kwanza kufuatia shambulizi zuri, mpira unakwenda nje
Dak ya 53, DRC wanaanza eneo la nyuma
Dak ya 52, Mohammed Issa na mpira, pasia kwa Msuva, unamkuta kipa wa Congo anaokoa kwa kupiga shuti kali

Dak ya 51, Msuuuuva, piga shuti kali lakini linaishia kwenye nyavu za nje, ilikuwa ni shambulizi moja zuri kwa Stars
Dak ya 50, Nyoni anacheza madhambi, mpira unapigwa kuelekea Stars, piga huku lakini DRC wanaudaka tena
Dak ya 49, Goli kiki, DRC wanaanza
Dak ya 48, Hatarii, Samatta anamtengeneza pasi muruuua kabisa Msuva na anadondoshwa ndani ya eneo la penati boksi, Mwamuzi anasema hakuna penati.
Dak ya 47, Samatta anapasia kwake Yondani, kwake Samatta tena, mabeki wa DRC wanamchezea faulo Samatta, mpira unapigwa kuelekea DRC
Dak ya 46, Ma

No comments:

Post a Comment