TUMUSIFU BWANA

prop

Saturday 5 May 2018

Msuva awatoa wasiwasi wachezaji wa Yanga sc Algeria zidi ya mechi yao ya kesho

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kudownload APP YETU BOFYA HAPA, Au ingia playstore tafuta KALAMBO NEWS kisha bofya install.
Na George Mganga


Mtanzania Simon Msuva anayecheza soka la kimataifa nchini Morocco katika klabu ya Difaa El Jadidi, leo amekutana na wachezaji wa kikosi cha Yanga mjini Algiers, Algeria.

Msuva amepataa wasaa wa kuwatembelea wachezaji hao kwa madhumuni ya kuwajulia hali wakiwa wanasubiria mechi ya mkondo wa kwanza ya Kombe la Shrikisho Afrika dhidi ya USM Alger itakayopigwa kesho.




Msuva alikuwa Algiers na kikosi cha Difaa El Jadidi kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo timu yake jana ilikuwa na kibarua dhidi ya MC Alger katika mtananage ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.

Winga huyo aliwahi kuichezea Yanga kabla ya kutimkia Uarabuni kujiunga na Difaa ambayo anaitumikia kwa sasa.

Kikosi cha Yanga kesho kitakuwa kinashuka dimbani kwa ajili ya kukipiga na USM Alger, mechi ikitarajiwa kuanza majira ya saa 4 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
05
May
2018

No comments:

Post a Comment